Majirani wa Tanzania, DR Congo wamewagalagaza
majirani zao Congo, maarufu kama Congo Brazzaville kwa kuwachapa mabao 4-2
licha kuwa walianza kwa kufungwa.
DR Congo sasa wamefuzu hadi nusu fainali ya
michuano ya Afcon.
Congo ambao walifuzu baada ya Caf kuwaengua
Rwanda, walitangulia na kufunga mabao 2-0 wakiwaacha nyuma DR Congo ambao
baadaye walipambana vilivyo na kufunga mabao manne.
Kipindi cha pili kilionekana kuwa mali ya DR Congo
na washambuliaji wake Thievy Bifouma aliyefunga mabao mawili, Dieumerci Mbokani
na wenzake wakionekana kuwapa wakati mgumu majirani na wapinzani wao wakubwa.
0 COMMENTS:
Post a Comment