March 4, 2015


Uongozi wa Azam FC, umeanza juhudi za kusaka kocha msaidizi kwa ajili ya kikosi chao.


George ‘Best’ Nsimbe amepewa nafasi ya kuendelea kama kocha mkuu, huku kocha msaidizi akitafutwa.

Habari za uhakika kutoka Azam FC zimeeleza kuwa tayari juhudi za kumsaka kocha msaidizi zimeanza.

"Kweli kuna makocha kadhaa ambao tunafanya nao mazungumzo, Best ndiye atakuwa kocha mkuu," kilieleza chanzo cha uhakika.

Best raia wa Uganda amechukua nafasi ya aliyekuwa Kocha Mkuu, Joseph Omog raia wa Cameroon.

Uongozi wa Azam FC, umeonekana kuwa na nafasi nzuri ya kumuachia Best achukue jahazi hilo.


Omog ametimuliwa kibarua baada ya Azam FC kung’olewa na El Merreikh katika Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kufungwa jumla ya mabao 3-2.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic