Chelsea
sasa imeamua, iko katika mipango ya kumnasa kiungo Gareth Bale na imetenga
pauni milioni 75.
Iwapo
itakubaliana na Real Madrid kumnasa Bale kwa kitita hicho itakuwa ni rekodi
mpya ya usajili nchini England.
Taarifa
kupitia gazeti la Dailymail la Uingereza zimeeleza kuwa Real Madrid tayari wana
taarifa hizo za Chelsea lakini wanaona angalau Bale abaki msimu mmoja zaidi.
Bale
alitua Madrid kwa kitita cha pauni milioni 86 akitokea Tottenham na kumfanya
awe mchezaji ghali zaidi duniani.
Raia huyo
wa Wales, tayari ameanza kuonyesha cheche zake akiwa na Madrid na jana
aliifungia timu yake ya taifa mabao mawili wakati ikiichapa Esrael kwa mabao
3-0 katika mechi ya kuwania kucheza michuano ya Ulaya.
0 COMMENTS:
Post a Comment