Na
Saleh Ally
SIMBA
itakuwa na kazi ngumu kuhakikisha inalipa kisasi cha kufungwa mabao 2-0 katika
mechi ya Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya watani wao, Yanga.
Simba
inakutana na Yanga katika mechi ya pili ya Ligi Kuu Bara msimu wa 2014-15 baada
ya mechi ya kwanza ya msimu huu kumalizika kwa suluhu.
Kikosi
cha Simba chenye wachezaji kadhaa wenye uwezo wa kubadili matokeo kupitia uwezo
wao binafsi, kitakuwa na kazi ngumu ya kufanya mabadiliko ya kuhakikisha kinapata
ushindi.
Tofauti
na hali ambayo imekuwa ikionekana kama Simba imekuwa ikiionea Yanga, takwimu
zinaonyesha Yanga ndiyo imefanya vizuri zaidi ya Simba katika mechi tano
zilizopita.
Hapa
tunazungumzia mechi za Ligi Kuu Bara na si zile za Kombe la Nani Mtani Jembe
ambalo Simba ndiyo wababe zaidi ya watani wao Yanga.
Katika
Nani Mtani Jembe, Yanga na Simba zimeshakutana mara mbili na mara zote Yanga
wamekiona cha moto kwa kuchapwa mara mbili.
Katika
mechi ya kwanza iliyopigwa Desemba 21, 2013, Yanga walikutana na kipigo cha
mabao 3-1 na Simba kubeba ubingwa. Mechi ya pili, Desemba 13, 2014, Simba
wakaendeleza ubabe kwa kushinda mabao 2-0.
Ukiachana
na mechi hizo za Nani Mtani Jembe, ukirejea kwenye Ligi Kuu Bara, Simba
haijashinda hata mara moja katika michezo mitano iliyopita.
Mchezo
wa sita kabla, ni ule ambao Simba ilitoa adhabu ya kipondo cha mabao 5-0 kwa
watani wao hao ikiwa ni mechi ya kufunga msimu wa 2011-12 iliyopigwa Mei 6,
2012.
Kwa
hesabu nzuri, unaweza kusema Simba haijaifunga Yanga katika Ligi Kuu Bara kwa
misimu mitatu hadi sasa.
Kwani
kuanzia msimu wa 2012-13, katika mechi mbili za ligi hiyo, mechi ya kwanza timu
hizo zilikutana Oktoba 3, 2012 na zikatoka sare ya bao 1-1, Simba ikianza
kupata bao la mapema kupitia kwa Amri Kiemba katika dakika 4, lakini Said
Bahanuzi akaisawazishia Yanga kwa mkwaju wa penalti katika dakika ya 65.
Watani
wakafunga msimu kwa Yanga kuifunga Simba katika mechi ya pili kwa mabao 2-0
mnamo Mei 18, 2013, wafungaji wakiwa ni Hamis Kiiza na Dider Kavumbagu.
Yanga
wakaondoka msimu huo wakiwa wababe na msimu uliofuata ni 2013-14. Mechi ya
kwanza Oktoba 20, 2013, ngoma ikalala 3-3. Kama unakumbuka Yanga waliongoza 3-0
hadi mapumziko, wengi wakajua Mnyama ‘anakula’ 5, Simba ‘wakachomoa’ zote!
Mechi
ya pili ya kufunga msimu, ikapigwa Aprili 19, 2014 na Simba wakaanza kufunga
katika dakika ya 75 kupitia kwa Haruna Chanongo, Yanga kupitia kwa Simon Msuva
wakasawazisha katika dakika ya 86.
Msimu
wa tatu ni huu wa 2014-15 ambao timu hizo zilikutana mapema zaidi, ilikuwa
Oktoba 18, 2014 baada ya kila timu kuwa imecheza mechi tatu na zikamaliza kwa suluhu.
Mechi
ya keshokutwa ni ya sita inayokamilisha misimu mitatu kamili kwa kuwa kila
msimu, timu hizo zinakutana mara mbili.
Takwimu
zinaonyesha hivi, katika mechi tano za misimu mitatu zilizokutana timu hizo,
Yanga imeshinda mara moja na sare nne.
Simba
ina kazi hiyo ya kulipa kisasi cha ubabe wa Ligi Kuu Bara kwa kuwa Yanga
angalau wanaongoza kwa kuwa na ushindi mmoja uliowapa pointi tatu.
Ndani
ya misimu mitatu, Simba haijawahi kuifunga Yanga katika Ligi Kuu Bara, huenda
keshokutwa wanaweza kubadilisha mambo.
MECHI 5 ZILIZOPITA ZA MISIMU MITATU:
Yanga
1-1 Simba
Simba
0-2 Yanga
Simba 3-3 Yanga
Yanga
1-1 Simba
Yanga
0-0 Simba
MABAO
YA KUFUNGA:
Simba
5
Yanga
7
MECHI
5:
Yanga
(Shinda 1, Sare 4, Poteza 0)
Simba
(Shinda 0, Sare 4, Poteza 1)
0 COMMENTS:
Post a Comment