March 27, 2015


Shirikisho la Mpira Soka Tanzania (TFF), limetangza viingilio vya mchezo wa siku ya Jumapili kati ya Taifa Stars dhidi ya The Flames (Malawi) utakaochezwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza kuwa ni tsh. 5,000 mzunguko na tsh. 12,000 kwa jukwa kuu.


Kuelekea mchezo huo wa jumapili kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) inayodhaminiwa na Bia ya Kilimanjaro, kimeendelea na mazoezi katika Uwanja wa CCM Kirumba huku wachezaji wake wote wakiwa na ari na morali ya juu tayari kwa kuwakabili the Flames.

Taifa Stars iliyo chini ya kocha mkuu Mart Nooij iliwasili jijini Mwanza siku ya jumanne na kufikia katika hoteli ya La Kairo iliyopo eneo la Kirumba,
ikiwa na kikosi  kamili kwa ajili ya mchezo huo wa kirafiki wa Kimataifa uliopo kwenye kalenda ya FIFA.

Maandalizi ya mchezo kwa upande wa Taifa Stars yamekamilika, timu imekua ikifanya mazoezi katika uwanja wa CCM Kirumba ambao ndio uwanja utakaotumika kwa mchezo.

Wachezaji waliopo jijini Mwanza ni , Aishi Manula, Mwadini Ali, Shomari Kapombe, Erasto Nyoni, Aggrey Morris, Oscar Joshua, Nadir Haroub, Salim Mbonde, Haji Makame, Hassan Isihaka na Abdi Banda.

Wengine ni Mwinyi Kazimoto, Haroun Chanongo, Mrisho Ngasa, Salum Abubakar, Amri Kiemba, Frank Domayo, Said Ndemla, John Bocco, Juma Luizio, Thomas Ulimwengu na Mbwana Samatta.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic