March 25, 2015


Kiungo mwenye kasi wa Yanga, Simon Happygod Msuva amefikisha mabao 11 baada ya kufunga mawili leo.

Msuva amefunga bao lake la 11 katika mechi ya Ligi Kuu Bara dhidi ya JKT Ruvu kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar.

Msuva alianza kufunga bao la katika dakika 34 kwa mkwaju wa penalti na kufanikiwa kumfikia mshambuliaji Didier Kavumbagu wa Azam FC. Lakini baadaye akafunga bao la tatu kwa Yanga leo na la pili kwake hivyo kufikisha mabao 11.


Kavumbagu raia wa Burundi amekuwa akiongoza kwa ufungaji tokea kuanza kwa ligi hiyo.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic