Simba inaanza mazoezi rasmi Jumatatu kujiwinda dhidi ya Stand United.
Kocha wa Simba, Goran Kopunovic amesema wamewapumzisha wachezaji wake siku moja.
"Leo kulikuwa na mazoezi, Jumapili (kesho) itakuwa ni mapumziko. Halafu rasmi Jumatatu tunarudi kazini.
"Mechi zote zilizobaki ni muhimu kwetu, kidogo tunataka kuonyesha mambo tofauti na ikiwezekana kushinda mfululizo.
"Iwapo tutashinda mfululizo, tutajiweka katika nafasi nzuri hata katika kugombea ubingwa," alisema.
0 COMMENTS:
Post a Comment