Mkurugenzi wa
Uhusiano wa Yanga, Jerry Muro amesema wanaondoka Jumatano na mechi hiyo
itapigwa Jumapili ijayo.
Yanga inatarajia kwenda Zimbabwe kuwavaa FC Platinum katika mechi ya pili ya Kombe la Shirikisho.
“Sasa tunajua pambano
litacheza tarehe nne. Awali tulikuwa hatuna uhakika.
“Kwa hiyo tunaondoka
tarehe moja kwenda Zimbabwe kwa ajili ya mechi hiyo,” alisema Muro.
Yanga ilianza vizuri
mechi ya kwanza baada ya kuichapa mabao 5-1.
Ili kusonga mbele
inahitaji sare ya aina yoyote.
0 COMMENTS:
Post a Comment