April 24, 2015

Kiungo wa Yanga, Simon Msuva amezidi kupaa katika upachikaji mabao katika Ligi Kuu Bara baada ya kufunga mabao mawili leo na kufikisha 16.


Msuva amezidi kujichimbia kileleni katika nafasi ya ufungaji bora lakini bao alilofunga kwa kichwa cha kuchupa katika mechi dhidi ya Ruvu Shooting ndiyo limekuwa gumzo zaidi.

Bao hilo limekuwa likifafanishwa na lile alilofunga mshambuliaji Robin van Persie wa Man United wakati akiitumikia timu yake ya taifa ya Uholanzi wakati wa Kombe la Dunia nchini Brazil, mwaka jana.

Msuva naye alichupa kuiwahi krosi safi ya Haruna Niyonzima na kupachika bao hilo.

Baada ya hapo mashabiki wamekuwa wakijadili kwenye mitandao mbalimbali wakijaribu kulilinganisha bao hilo na lile la van Persie.

Anayemfuatia Msuva kwa wingi wa mabao ni Amissi Tambwe ambaye amefunga bao moja leo na kufikisha 11.

Hivyo kufanya wachezaji hao wawili wa Yanga kumpiku Didier Kavumbagu wa Azam FC mwenye mabao 10 ambayo yalimfanya aongoze kwa muda mrefu.


Mwingine mwenye mabao 10 ni Emmanuel Okwi aliyepachika Hat Trick katika mechi yao ya mwisho dhidi ya Mgambo Shooting, juzi.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic