Beki wa zamani wa Arsenal, Sol Campbell ameamua
kuliuliza jumba lake la kisasa lililo jijini London.
Taarifa zimeeleza Campbell ameamua kuliuza jumba
hilo kwa kitita cha pauni milioni 6 na inaelezwa ni kutokana na kutokuwa katika
hali nzuri kifedha.
Imeelezwa Campbell aliuza jumba lake jingine
mwanzoni mwa mwaka huu kwa kitita cha pauni milioni 20.
Hata hivyo kumekuwa na taarifa kwamba Campbell
ameamua kuliuliza jumba hilo akiwa katika harakati za kukwepa kodi.
Beki huyo wa zamani wa Arsenal ameendelea kukaa
kimya kuhusiana na hilo huku mipango ya mauzo ikiendelea.
CAMPBELL AKIWA NA MKEWE FIONA |
0 COMMENTS:
Post a Comment