May 6, 2015

Beki wa zamani wa Barcelona, Eric Abidal ameamua kufungukam mambo mengi kuhusiana na uginjwa wa kansa.

Pamoja na mengi, ameendeleza jambo ambalo limewashitua wengi baada ya kusema beki mwenzake wakati huo, Dani Alves alikuwa tayari kumzawadia moja ya ini lake.
Abidal raia wa Ufaransa aliambiwa na ugonjwa wa kansa kwenye ini mwaka 2011 alipokwenda hospitai kufanyiwa vipi vya kawaida.

“Sikujua kama nilikuwa mgonjwa, nilikuwa fiti lakini ilikuwa ni kawaida kwenda hospitali na kufanyiwa vipimo fulani baada ya muda fulani.

“Nikaambiwa ni mgonjwa, hakika nilishituka sana. Lakini nikaanza matibabu.

“Wakati fulani, Alves alisema alikuwa tayari kutoa ini lake kwangu.

“Lakini nikaona si sahihi, lilikuwa ni jambo zuri lakini hapa kwa kweli. Sikukubaliana naye,” alisema Abidal wakati akihojiwa na DailyMail la Uingereza.

Kwa sasa anajishughulisha na Abidal Foundation inayofanya kazi ya kusaidia kuwatibu watoto wanaosumbuliwa na ugonjwa wa kansa.






0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic