Mashabiki
wengi wikiendi iliyopita walishtushwa kuona beki kisiki wa Azam FC, Pascal
Serge Wawa akitolewa kipindi cha pili cha mchezo huo wakati yeye ndiye nguzo ya
Azam, lakini imebainika kuwa alicheza mechi hiyo dhidi ya Simba akiwa anaumwa
Malaria.
Wawa raia wa
Ivory Coast, alifanikiwa kumdhibiti Emmanuel Okwi lakini baadaye nafasi yake
ilichukuliwa na kiungo, Mudathir Yahya.
Kuhusu suala
hilo, Kocha Mkuu wa Azam, George ‘Best’ Nsimbe alisema: “Sikuwa na jinsi,
ilibidi tumtoe Wawa baada ya kusema hawezi kuendelea, najua alikuwa
akisumbuliwa na malaria jana (Jumamosi), lakini asubuhi alisema yupo fiti ndiyo
maana nikampanga.”
0 COMMENTS:
Post a Comment