RAIS WA SIMBA, EVANS AVEVA AKITOA HUTUBA, HUKU MAKAMU WAKE, GEOFREY NYANGE 'KABURU' AKIWAZA JAMBO FULANI... |
Na Saleh Ally
KLABU ya Simba imeanza
usajili kwa ajili ya msimu ujao, ikiwa imepania kufanya mabadiliko makubwa na
lengo kubwa ni kukiweka kikosi chake katika hali itakayorejesha makali ya
Simba.
Simba haijashiriki
michuano ya kimataifa kwa misimu mitatu sasa na inaonekana kama watalala, basi
itakula kwao kwa msimu mwingine.
Mambo yalivyo kwa
uhakika, si mazuri. Juhudi za kuhakikisha kikosi kinakuwa bora zinahitaji mambo
mengi sana lakini muda na fedha, vyote havikwepeki.
Bado kuna utulivu,
ushirikiano na kuaminiana. Lengo la yote ni kutimiza mambo muhimu yanayotakiwa
kwa ajili ya kuiimarisha Simba.
HANS POPPE AKIWA NA TALIB HILAL, MMOJA WA MAKOCHA WA ZAMANI WA SIMBA, PIA WALIOWAHI KUICHEZEA TIMU HIYO KWA MAFANIKIO. |
Jana nilizungumza
kuhusiana na Kamati ya Usajili ya Simba kupewa nafasi ya kufanya kazi yake na
si kila mjumbe wa kamati ya utendaji kuwa fundi na kutaka kufanya usajili, ili
mradi anajuana na wachezaji au makocha.
Wakati juhudi za kufanya
mabadiliko zinaendelea, kuna kila haja ya uongozi wa Simba na kamati yake ya
utendaji kwanza kukubali kwamba wana matatizo ambayo pia ni sehemu ya kuyumba
kwao.
Kwamba ili wabadilike, ni
lazima wayakubali na kuyafanyia kazi. La sivyo watafanya kila kitu halafu
mwisho itakuwa ni sawa na kutwanga maji kwenye kinu, maana hawatafanikiwa na
wataonekana kuwa wanaidanganya jamii ya Wanasimba.
Ndani ya uongozi wa
Simba, ukianzia viongozi hadi wajumbe wa kamati ya utendaji, kuna ubinafsi.
Wapo viongozi ambao wamekuwa wakitaka kuonekana au kujulikana zaidi ya wenzao.
Hawataki wengine
wajulikane. Wapo wengine wanafanya kazi sana, hata kuonekana kwao kunalingana
na wanachokifanya, lakini wapo wasiofanya lolote, wasingependa kuona wenzao
hata kama wanafanya kazi sana wanaonekana!
Mfano ambao
nafikiri unaweza kuwa chanzo cha mimi kuamua kuwaeleza Simba kuhusiana na
kukubali kupitia makosa yao ni lile sakata la kupatikana kwa mtu aliyeaminika
alikuwa akiwapa vitu wachezaji ambavyo vilionekana kuwaathiri.
Simba wamelificha sana
hili, sijui kwa nini wameamua kulifanya siri wakati ilibainika kiongozi wa
kuchaguliwa tena wa ngazi za juu, alibainika kuwapa wachezaji dawa ambazo
ziliwapunguza nguvu, wakashindwa kucheza kwa kasi waliyonayo kwa muda wote.
TULLY, MJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI NA KAMATI YA USAJILI YA SIMBA AKIZUNGUMZA NA KOCHA WA ORANDO PIRATES WAKATI SIMBA ILIPOWEKA KAMBI NCHINI AFRIKA KUSINI. |
Wao Simba wanajua hilo
ndiyo tatizo la wao kutoka sare nyingi kwa kuwa kila timu ilipofunga, kipindi
cha pili ilidorora na kuachia nafasi ya kusawazishiwa na baadaye kufungwa.
Uchunguzi wa viongozi wa
Simba ulifanyika, wakabaini hilo, wakamuweka chini daktari naye akakiri kwamba
alikuwa akipewa vitu na kiongozi fulani na kweli hata mpishi alikiri kuhusiana
na hilo!
Sijui sababu za wao
kuamua kukaa kimya na kulificha hilo? Lakini taarifa zinaeleza kuwa walimuweka
kiongozi huyo kiti moto, naye akaomba radhi akitoa utetezi usiokuwa na mashiko.
Kwangu kiongozi wa namna
hiyo ni hatari kabisa kwa Simba, kwangu bado siamini kama kweli anaipenda klabu
hiyo na sitakuwa tayari kumsikiliza hata siku moja akisema ana mapenzi na klabu
hiyo.
Huyo ana mapenzi na yeye
mwenyewe na ndiyo mfano sahihi wa ubinafsi ninaouzungumzia ambao Simba wakati
wanaanza usajili wa msimu huu lazima waukomeshe kwanza.
Nimekuwa nikijiuliza,
hata kama kweli kiongozi huyo amesamehewa wakati alidiriki kuihujumu timu
anayoipenda na kuiongoza, sasa anaendelea kuwa ndani ya kikosi, kweli ataacha
tabia hiyo au ataendelea kupanga mipango mingine ya kuiangusha?
Uongozi wa juu kwa
kushirikiana na kamati ya utendaji, wanapaswa kuwa makini kwa kuwa adui wa
ndani ni hatari maradufu kuliko adui wa nje.
Mmekubali kumbakiza
ndani, huenda kwa undugu, urafiki wenu au uungwana wenu tu, lakini mimi
nasisitiza, lazima muwe makini maradufu, mkubali makosa yenu ili muweze kufanya
vizuri zaidi.
Kwa wewe uliyekamatwa na
shutuma hii mbaya kabisa, kama kweli ulifanya basi jirekebishe na ubadilike
kweli, pia bahati yako sijakujua jina.
Kaka unazungumzia kitu unachokijua au unazungumzia habari za kijiweni na majungu!!? Sasahivi si wakati wa kuanza kuchafuana!!
ReplyDelete