MURO |
Mkuu wa Kitengo cha Habari cha Yanga, Jerry
Muro amesema kuwa mkuu wa kitengo kama chake upande wa Simba, Haji Manara
ameangukiwa na jumba bovu.
Muro amesema hayo akisisitiza kauli ya
kwamba Simba haijafanya vizuri lakini Manara amekuwa akiendelea kusema maneno
mengi.
Akizungumza mara tu baada ya kurejea
akitokea Tunisia alipoongozana na kikosi cha Yanga, Muro alisema Manara amekuwa
na maneno mengi wakati akijua Simba haina lolote msimu huu.
“Naye anazungumza sana, anajua jumba bovu
limemuangukia. Lakini anazuga tu,” alisema.
MANARA |
“Kuhusiana na suala la Yanga iifunge Azam
kwa ajili ya kuisaidia Simba, hilo ni suala la klabu na kesho tutalitolea
ufafanuzi.
“Tumeamua kufanya mkutano na waandishi
kuzungumzia masuala kadhaa ikiwemo safari yetu ya Tunisia. Lakini hilo pia
tutalitolea ufafanuzi,” alisisitiza Muro.
Yanga imetolewa katika michuano ya Kombe la
Shirikisho kwa kufungwa bao 1-0 na Etoile du Sahel ya Tunisia. Hivyo kuwa imeng’oka
kwa jumla ya mabao 2-1.
Msipange matokeo waziwazi nyie YANGA.
ReplyDelete1.YANGA
ReplyDelete2.AZAM
Simba wasubiri kwanza,wajifunze ubinadamu.
Uwezo wa kumfunga Azam sisi Yanga hatuna. Kwanza wana machungu ya kufungwa na simba, pili wanahitaji ushindi ili kuipata hiyo nafasi ya pili lakini muhimu zaidi Yanga morali yetu ipo chini sana baada ya kufungwa Tunisia na Simba kutuzomea sana.
ReplyDelete