May 30, 2015


 
MAVUGO
Kocha wa zamani wa Simba, Goran Kopunovic amesema iwapo Simba watafanikiwa kumnasa Laudit Mavugo, atatoa msaada mkubwa katika safu ya ushambuliaji.

Akizungumza na SALEHJEMBE, Kopunovic amesema Mavugo ni mmoja wa wachezaji wenye kiwango kizuri katika ushambuliaji.

“Ni mshambuliaji mzuri, ana kasi, nguvu, anapiga mashuti, pia mzuri wa mipira ya juu kutokana na mfumo unaotumiwa na kocha.
 
MAVUGO NA KOPUNOVIC
“Ninaamini ataongeza chachu ya Simba kuwa na safu nzuri ya ushambuliaji,” alisema Kopunovic ambaye ndiye alimpendekeza Mavugo raia wa Burundi.

Mavugo sasa ni mshambuliaji tegemeo wa Vital’O ya Burundi. Pia timu ya taifa ya Burundi na tayari yuko katika hatua nzuri ya mazungumzo na mshambuliaji huyo.


Kabla Mavugo aliwahi kufanya kazi pamoja na Kopunovic katika kikosi cha Polisi Rwanda.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic