Ligi Kuu ya Tanzania Bara
inatarajiwa kuendelea kesho kwa mchezo mmoja utakaopigwa katika dimba la Uwanja
wa Taifa jijini Dar es salaam, wenyeji timu ya Azam FC watawakaribisha Mabingwa
wapya wa ligi hiyo msimu huu timu ya Young Africans.
Mechi hiyo no. 141
itachezeshwa na mwamuzi wa kati Jacob Adongo kutoka Mara, akisaidiwa na washika
vibendera Frednand Chacha (Mwanza), Hellen Mduma (Dsm), huku mwamuzi wa akiba
akiwa ni Hussein Kalindo (Dsm) na Kamisaa wa mchezo huo ni Damian Mabena kutoka
Tanga.
Katika mchezo huo timu
ya Young Africans itakabidhiwa Kombe lake la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom
Tanzania bara msimu wa 2014/2015, na mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Waziri wa
Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo, Dr Fennela Mkangara.
Mchezo huo wa kesho
unatarajiwa kuanza majira ya saa 11 kamili jioni, kwa saa za Afrika Mashariki
na kati ili kutoa fursa kwa wadau, wapenzi na mashabiki wa mpira wa miguu
nchini kujitokeza kushudia mchezo huo pamoja na shamrashamra za kukabidhiwa
kikombe.
Young Africans
watakabidhiwa Kombe la Ubingwa wa Ligi Kuu ya Vodacom msimu huu na mgeni rasmi,
huku wadhamini wa ligi hiyo kampuni ya simu za mkononi ya Vodacom wakimkabidhi
zawadi mchezaji bora wa mwezi Aprili Mrisho Ngasa na fedha taslimu sh. millioni
moja.
0 COMMENTS:
Post a Comment