Kocha Mkuu wa
Yanga, Hans van der Pluijm atarejea nchini Juni 6 tayari kuanza kazi.
Yanga imejipanga
kuanza mazoezi kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya Juni 8 jijini Dar es
Salaam.
Mkuu wa Kitengo
cha Habari cha Yanga, Jerry Muro amesema Pluijm raia wa Uholanzi, mara moja
ataanza mazoezi na timu hiyo baada ya kurejea.
“Kocha kama
mnavyojua yuko mapumziko, baada ya kurejea ataanza kazi moja kwa moja. Lengo ni
kuanza maandalizi mapema kabisa,” alisema.
“Kuna michuano ya
Kagame, pia kuna michuano mingine ya kimataifa pia ligi kuu, hivyo lazima tuanza maandalizi
mapema.”
Yanga tayari
imeanza kufanya usajili kwa ajili ya kuimarisha kikosi chake ambacho pamoja na
michuano ya Kagame, kitashiriki ligi ya Mabingwa Afrika.
0 COMMENTS:
Post a Comment