Cristiano Ronaldo ni nomaaa, amepiga hat-trick nyingine
wakati Real Madrid ikiichinja Getafe kwa mabao 7-3 katika mchezo wake wa mwisho
wa La LiGa msimu huu.
Kwa mabao hayo Ronaldo amefikisha mabao 48 na
kufanikiwa kubeba tuzo ya Pichichi ya mfungaji bora ambayo amekuwa akikimbizana
na Lionel Messi wa Barcelona.
Kwake pia ni hat trick ya saba tokea ajiunge na
Real Madrid akitokea Manchester United. Hivyo ana jumla ya mabao 61 kwa msimu
mzima.
Kwa jumla ya mabao 61, Ronaldo amevunja rekodi
yake ya awali ya mabao 60 kwa msimu wa 2011-12.
Raul anaendelea kuongoza kwa kuwa mfungaji bora
zaidi Madrid kutokana na mabao yake 323 katika mechi 741 alizoichezea timu hiyo
wakati Ronaldo ambaye tayari ameichezea Madrid mechi 300 amefikisha mabao 313
akiwa amebakiza mabao 10 tu kumng’oa Raul.
0 COMMENTS:
Post a Comment