Simba imeendelea na mazoezi leo kwenye
Uwanja wa Chuo Kikuu jijini Dar es Salaam kujiwinda na mechi zilizobaki za Ligi
Kuu Bara.
Kocha Msaidizi wa Simba, Selemani Matola
amesema wanaendelea kupambana na wanachotaka ni kushinda mechi zilizobaki.
“Kwetu msimamo ni uleule, kupambana na
kushinda mechi zilizobaki. Hayo mengine yatafuatia tutaona.
“Katika soka hautakiwi kukata tamaa, unashindwa
mwisho kabisa na si sasa,” alisema Matola akionyesha kujiamini.
Simba walionekana na furaha na walifanya
mazoezi ikiwemo kucheza soka.
Mazoezi yao yalikuwa makali utadhani ni
mechi huku wachezaji wakikabana kwa nguvu “kijeshi”.
0 COMMENTS:
Post a Comment