Uongozi wa Simba umeonyesha umepania kuimarisha safu
yake ya ulinzi baada ya kumnasa beki wa JKT, Mohammed Faki, leo.
Fakli amesaini mkataba wa miaka miwili kuichezea Simba jijini Dar es Salaam na
Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe amethibitisha.
“Kweli Faki amesaini miaka miwili, hii ni sehemu ya
kuhakikisha tunaimarisha safu ya ulinzi,” alisema.
Faki aliichezea JKT kwa ufanisi mkubwa katika msimu
uliopita.
0 COMMENTS:
Post a Comment