Binadamu tajiri kuliko wote barani Aliko
Dangote amesema hajakata tamaa ya kuinunua klabu ya Arsenal.
Dangote raia wa Nigeria ambaye tayari
ana kiwanda cha saruji mkoani Mtwara nchini Tanzania, anakadiriwa kuwa na utajiri wa pauni
bilioni 10.4.
Tayari alitaka kununua shea za umiliki
wa Arsenal wakati aliyekuwa mkurugenzi na mmoja wa wamiliki Lady Nina
Bracewell-Smith alipoziuza mwaka 2010 lakini ikashindikana.
Lakini sasa Dangote amesisitiza yuko
tayari na anataka kuwa mmoja wa wamiliki wa Arsenal.
Kwa sasa milionea wa Kimarekani, Stan
Kroenke, ndiye mmiliki mkuu wa klabu hiyo.
Raia wa Uzbekistan, Alisher Usmanov naye
anamiliki asilimia 30 za shea za klabu hiyo maarufu England na duniani kote.
0 COMMENTS:
Post a Comment