KAZIMOTO |
Timu ya Al Markhiya ya
imekumbana na kipigo cha mabao 6-0 dhidi ya Al Rayyan katika mechi iliyochezwa mwishoni mwa wiki iliyopita.
Al Markhiya ndiyo timu
anayoichezea Mtanzania Mwinyi Kazimoto, ilikumbana na kipigo hicho katika Ligi
ya Qatar ikiwa ugenini.
Pamoja na kipigo hiyo, Al
Markhiya inaendelea kubaki katika nafasi ya tatu ikiwa na pointi 31.
Al Mesaimeer inaongoza ligi
hiyo kwa kuwa na pointi 44 ikifuatiwa na Al Mu’aidar yenye pointi 40.
Kipigo hicho kutoka kwa
timu isiyo top 5, kimeifanya Al Markhiya kuzidi kupoteza nguvu angalau ya
kuwania ubingwa.
Sare ni nne, moja imetoka
ikiwa nyumbani na tatu ikiwa inacheza ugenini.
Safu yake ya ushambuliaji
imefunga mabao 37, lakini safu ya ulinzi imeonekana kutokuwa imara kwa kuruhusu
mabao 31.
0 COMMENTS:
Post a Comment