May 23, 2015

MAVUGO (KUSHOTO)

Simba imeamua kumsubiri mshambuliaji Laudit Mavugo amalize mechi mbili katika kikosi chake cha Vital’O kabla ya kuja kujiunga nayo kwa ajili ya majaribio.


Lakini vurugu za kumpinga Rais Pierre Nkurunziza ambaye anataka kugombea kwa muhula wa tatu, ndizo zimechangia zaidi Simba kufanikisha jambo hilo.

Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Simba, Zacharia Hans Poppe ambaye amekuwa akilifuatilia suala hilo kwa karibu, amekiri vurugu hizo zimechangia kuongeza ugumu wa jambo hilo.

“Kweli hapa kuna suala la kusubiri amalize ligi na zimebaki mechi mbili. Tumefanya mazungumzo na klabu yake, pia imani yangu mambo yatakwenda vizuri.

“Lakini mambo mengine yamekuwa yakikwamishwa na vurugu zinazoendelea Burundi,” alisema Hans Poppe ambaye ndiye ‘Jembe’ la usajili la Simba.

Mavugo amekuwa tegemeo katika safu ya ushambuliaji wa Vital’O na aliwahi kufanya kazi na Kocha Goran Kopunovic.

Kopunovic ndiye aliyempendekeza Mavugo kwa kuwa alikuwa mchezaji wake akiwa Polisi Rwanda. Lakini mwisho yeye ameondoka baada ya kutaka apewe dau la Sh milioni 100 ili asaini mkataba mpya, jambo ambalo Simba hawakukubaliana naye.

Simba imekuwa haina straika wa uhakika wa ‘kucheka’ na nyavu mara baada ya kumruhusu Amissi Tambwe aondoke.

Tambwe aliondoka Simba akiwa mchezaji huru, Yanga ikaokota ‘dodo’ na sasa ni kati ya wachezaji inaowategemea katika ufungaji.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic