Shirikisho la Soka Afrika (CAF), limewateua waamuzi wa kike kutoka Tanzania kuchezesha
mchezo wa kuwania kufuzu kwa Fainali za Kombe la Dunia kwa Wanawake U-20 mwaka
2016 kati ya Congo DR dhidi ya Gabon.
Mchezo huo unatarajiwa
kuchezwa jumamosi tarehe 09.05.2015 jijini Kinshasa, DR Congo, mwamuzi
wa kati ni Jonesia Rukya, akisaidiwa na washika vibendera Dalila Jafari na
Sophia Mtongoli huku mwamuzi wa akiba akiwa ni Hellen Mduma.
Wakati huo huo
Elizabeth Kalinga ameteuliwa kuwa kamisaa wa mchezo kati ya Kenya dhidi ya
Botswana kuwania kufuzu kwa michuani ya Olympiki, mchezo utakaofanyika Mei 31,
2015 nchini Kenya.
0 COMMENTS:
Post a Comment