May 27, 2015


Wakati harakati za usajili zinazidi kupamba moto, mabingwa wa Tanzania Bara, Yanga wanaonekana kuwa ndiyo waliomwaga fedha nyingi zaidi katika kipindi cha usajili.


Yanga wamemwaga zaidi ya Sh milioni 195 katika fedha zao ambazo wametumia kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao na watamwaga zaidi ya hizo hadi watakapokuwa wamemaliza.

Gharama zinaweza kufikia zaidi ya Sh milioni 200 hadi sasa kama itajumlishwa na fedha walizowatumia wachezaji kwa ajili ya usafiri kutoka katika miji ya Mbeya, Zanzibar na pia kuwasafirisha wengine.

Wako ambao waliboresha mikataba yao na wengine wapya ambao tayari wameishatua Jangwani kwa ajili ya msimu ujao.

Kwa upande wa Simba, nao wanaonekana kujitutumua kwani katika fedha kwa ajili ya kuimarisha kikosi chao ukianzia zile za Jonas Mkude hadi sasa, tayari wametoa zaidi ya Sh milioni 165.

Simba wameboresha baadhi ya mikataba ya wachezaji wao lakini inaonekana pia bado wanaweza kufikia Sh milioni 200 na zaidi kwa kuwa bado wanahitaji kuboresha mkataba wa Ramadhani Singano ‘Messi’, Ivo Mapunda na pia kusajili wachezaji wapya.

Yanga (Sh milioni 195):
Deus Kaseke kutoka Mbeya City (Sh milioni 35), Haruna Niyonzima (Sh milioni 70), Mbuyu Twite (Sh milioni 30), Deogratius Munish ‘Dida’ (Sh milioni 20) na Benedict Tinocco kutoka Kagera (Sh milioni 20) na Haji Mwinyi Mgwali kutoka KMKM (Sh milioni 20).

Simba (Sh milioni 165):
Jonas Mkude (Sh milioni 60), Said Ndemla (Sh milioni 30), Hassan Isihaka (Sh milioni 30), Paul Mwalyanzi kutoka Mbeya City (Sh milioni 25), William Lucian ‘Gallas (Sh milioni 20).


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic