Mtangazaji maarufu wa
Clouds FM, Millard Ayo leo alifanya ziara fupi katika gazeti maarufu la michezo
la Championi.
Millard alifanya ziara
hiyo kwa mwaliko wa Mhariri Kiongozi wa Championi, Saleh Ally “Jembe”.
Mtangazaji huyo alipata
nafasi ya kuelezewa namna unavyokuwa uandaaji ya gazeti hilo la michezo hadi
utengenezaji.
Baada ya hapo
alibadilishana mawazo na waandishi pamoja na wahariri wa gazeti hilo kabla ya
kutembelea sehemu nyingine za Global Publishers pamoja na magazeti yake.
Millard ni kati ya
wadau wa michezo na amekuwa akijipatia mashabiki na wasikilizaji wengi wa
kipindi chake kutokana na umakini wake, pia tabia yake ya kujituma.
Mtangazaji huyo ambaye
pia ni mdau wa michezo na amekuwa akitupia stori za michezo kupitia mtandao
wake wa www.millardayo.com, amesema
amejifunza mambo mengi katika ziara yake hiyo fupi.
0 COMMENTS:
Post a Comment