NIZAR DAKIKA CHACHE BAADA YA AJALI HIYO MBAYA. |
Kiungo wa zamani wa
Yanga, Nizar Khalfan amenusurika na ajali mbaya ya gari iliyotokea eneo la Kibaigwa mkoani
Dodoma.
Imeelezwa, Nizar
alikuwa pamoja na kipa mpya wa Mwadui FC, Shabani Kado ambaye ni kipa bora
Tanzania Bara.
Hata hivyo, juhudi za
kuwapata hazikufanikiwa baada ya mtoa habari kueleza wote wamenusurika katika ajali hiyo iliyohusisha gari aina ya Mitsubish walilokuwa wanalitumia.
Baadaye Nizar ambaye
pia ametua Mwadui FC alitupia picha kwenye mtandao wa kijamii akieleza
amenusurika.
“Tunamshukuru Mungu
hadi sasa tuko salama,” alisema.
Taarifa zinaeleza
wawili hao walikuwa safari kwenda Shinyanga kujiunga na timu yao mpya ya Mwadui
FC kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao.
0 COMMENTS:
Post a Comment