June 29, 2015

NIZAR DAKIKA CHACHE BAADA YA AJALI HIYO MBAYA.
Kiungo wa zamani wa Yanga, Nizar Khalfan amenusurika na ajali mbaya ya gari iliyotokea eneo la Kibaigwa mkoani Dodoma.


Imeelezwa, Nizar alikuwa pamoja na kipa mpya wa Mwadui FC, Shabani Kado ambaye ni kipa bora Tanzania Bara.

Hata hivyo, juhudi za kuwapata hazikufanikiwa baada ya mtoa habari kueleza wote wamenusurika katika ajali hiyo iliyohusisha gari aina ya Mitsubish walilokuwa wanalitumia.

Baadaye Nizar ambaye pia ametua Mwadui FC alitupia picha kwenye mtandao wa kijamii akieleza amenusurika.

“Tunamshukuru Mungu hadi sasa tuko salama,” alisema.

Taarifa zinaeleza wawili hao walikuwa safari kwenda Shinyanga kujiunga na timu yao mpya ya Mwadui FC kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic