July 6, 2015


Mshambuliaji Kpah Sherman wa Yanga, amesema msimu ujao lazima atumie jezi namba 10, iliyokuwa ikimilikiwa na straika Jerry Tegete kwa muda klabuni hapo, huku jezi hiyo ikimfanya Sherman kuwa mchezaji pekee aliyebadilisha jezi mara nyingi kuliko mchezaji yeyote.


Tangu ajiunge na Yanga akitokea Cetinkaya ya Cyprus msimu uliopita, nyota huyo ametumia jumla ya jezi nne, akifuatiwa na Amisi Tambwe aliyebadilisha jezi mara tatu ndani ya msimu mmoja akiwa na Yanga.

Wakati anasajiliwa, Sherman alianza kwa kuvaa jezi namba 25, kisha kubadilisha na kuvaa namba 29 kabla ya kuhamia jezi ya ‘nuksi’ namba 9 ambayo aliitumia hadi kumalizika kwa msimu uliopita.

Sherman alisema kwa muda mrefu aliitamani jezi namba 10, lakini ilikuwa ikitumiwa na mmoja wa wachezaji wakongwe klabuni hapo, hivyo aliamua kutulia huku akiumia kwa kuwa anaamini ina bahati kwake.
  
“Namba 10 ndiyo jezi yangu, niliipenda tangu zamani, lakini nilipofika hapa, bahati mbaya nilikuta ikitumiwa na mtu wa siku nyingi klabuni (Tegete), hivyo sikuwa na namna.

“Ndiyo maana baada ya kusikia kwa sasa iko huru, sikutaka kuipoteza tena, nikaiomba, naamini msimu ujao ndiyo itakuwa jezi yangu,” alisema Mliberia huyo.

Tambwe wakati anajiunga na Yanga alianzia jezi namba 29, kisha 19 kabla ya kuchukua jezi ya Mrisho Ngassa namba 17, ambayo anasema ndiyo jezi yake tangu aanze soka na aliitumia kila alikopitia.



0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic