July 30, 2015


Na Saleh Ally
TIMU nne zimebaki katika michuano ya Kombe la Cecafa inayoendelea na Tanzania imebaki na timu moja timu.


Wakati michuano inaanza, Tanzania Bara ilikuwa na timu mbili ambazo ni Azam FC na Yanga na Zanzibar ilikuwa na timu moja, KMKM.

Yanga na KMKM wametangulia, wameng’olewa katika michuano hiyo na sasa Watanzania wamebakiza timu moja.

Zilizobaki zinatokea Kenya-Gor Mahia, Uganda-KCCA na Al Khartoum ya Sudan.

Kama ni Mtanzania mzalendo, hakika atakuwa na hamu ya kuona kombe hilo linabaki nyumbani na timu pekee inayoweza kufanya hivyo ni Azam.

Azam ina uwezo wa kuingia fainali kwa kuwa hii si mara ya kwanza, mwaka 2010 iliingia ikiwa na Yanga, ikapoteza.

Safari hii ndiyo timu bora kabisa ya mashindano hadi zinabaki hizo nne kwa kuwa haijafungwa hata bao moja ndani ya dakika 90.

Maana yake ni timu yenye uwezo wa kufanya vizuri. Kilichobaki ni kuhakikisha inaungwa mkono kwa nguvu zote.

Jiulize mara mbili, kama wewe kweli ni Mtanzania, unafurahi vipi kuona kombe linachukuliwa Gor Mahia ambayo itawapelekea Wakenya au KCCA iwapelekee Waganda.

Rekodi za michuano hiyo zinaonyesha Simba imechukua mara 6 ambayo ni nyingi zaidi. Inafuatiwa na Yanga na Gor Mahia.

Sasa unataka Wakenya au Wasudan waende nalo? Ili iweje? Kwa faida ya nani? Nafikiri kuna kila sababu ya kuiunga mkono Azam FC.

Lakini tuhakikishe inasonga hadi fainali na kubeba kombe hilo kwa kuwa hatuna uwezo wa kuibadilisha isiwe timu ya Tanzania.

Azam FC ni ya mwekezaji Mtanzania, hivyo hatuna uwezo wa kulibadili hilo na huu ndiyo wakati wa kuonyesha uzalendo.

Si lazima kwa kila mtu afanye hivyo, anayeshindwa anaweza kubaki nyumbani. Anayeona ni muhimu kuunga mkono aende uwanjani na kuiunga mkono Azam FC kutoka Tanzania.



1 COMMENTS:

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic