Mkuu
wa Mkoa wa Manyara Dokta, Joel Bendera ameipongezs TFF kwa kuandaa mashindano
ya ya Taifa ya vijana wenye umri chini ya miaka 13 (U-13), na maandalizi
ya timu hiyo kwa ajili ya kuwania kufuzu kwa fainali za Afrika za vijana chini
ya miaka 17 zitakazofanyika mwaka 2019 nchini Tanzania.
Bendera
amesema hiyo ndiyo njia sahihi ya kuelekea kwenye mafanikio pia amepongeza
juhudi za Chama cha Soka mkoa wa Manyara na TFF kwa kuandaa kozi za makocha na
waamuzi, akisema huo ndiyo uwekezaji mkubwa katika maendeleo ya soka mkoani
Manyara.
Aidha
aliwaasa makocha kutumia mbinu za kisasa za ufundishaji soka walizozipata
kwenda kuendeleza vipaji vya wachezaji watakaowafundisha.
Pia
Bendera amewahakikishia wakazi wa Manyara atahakikisha wanaandaa vipaji
vitakvyowawezesha kuwa na timu bora itakayowakilisha mkoa wa Manyara.
0 COMMENTS:
Post a Comment