July 6, 2015

MAVUGO...
Beki wa zamani wa Simba, Mrundi, Said Kokoo, amewapambanisha kwa kuwachambua kwa kina Warundi wenzake, straika wa Yanga, Amissi Tambwe na yule wa Simba anayetarajiwa kutua hivi karibuni, Laudit Mavugo na kuweka wazi kuwa Mavugo ni noma.


Mavugo na Tambwe wote ni raia wa Burundi, hivyo wanatarajiwa kuonyeshana kazi kwa kushindana katika kuzisaidia timu zao kwenye mechi za ligi kuu kwa kuwa wanajuana vizuri, huku pia uhasama wao ukichangiwa na kuwa kwenye timu tofauti ambazo ni mahasimu wakuu hapa Bongo.
 
TAMBWE AKIWA MSUVA...
Beki huyo ambaye kwa sasa maskani yake ni hapa nchini, alisema kuwa anawafahamu vizuri wachezaji wote hao kwani amekuwa nao karibu na kuwafuatilia kwa kipindi kirefu mpaka hapa walipofikia, hivyo amebaini uzuri na ubora wa kila mmoja.

Alisema kuwa sifa alizonazo Mavugo zinamfanya ampige ‘bao’ Tambwe kwani aina yake ya uchezaji ambayo ni ya kasi inamruhusu kupiga chenga nyingi za maudhi na kufunga kwa ufundi mkubwa lakini Tambwe vitu hivyo hana.

Aliongeza kuwa, japo Tambwe kuna vitu anamzidi Mavugo ikiwemo uzoefu, kucheza kwa kujituma mwanzo mwisho pamoja na ujanja wa kukaa kwenye nafasi nzuri za kufunga, lakini hivyo vinaweza kufanywa na Mavugo kadiri atakapozidi kukomaa katika soka.
 
KOKOO (KUSHOTO) WAKATI AKIKIPIGA...
“Wote ni wachezaji wazuri japo wanatofautiana, Tambwe ni mzuri katika kufunga lakini Mavugo ni mzuri zaidi kwani anafunga, ana spidi, chenga nyingi, ndiyo maana Burundi alikuwa mfungaji bora mara mbili,” alisema Kokoo.

Mavugo ndiye mfungaji bora katika Ligi Kuu ya Burundi baada ya kuzifumania nyavu mara 34.


 “Tunamshukuru Mungu kwani muda wowote kuanzia sasa, Mavugo atatua nchini kwa ajili ya kuungana na kikosi chetu baada ya kufanikiwa kuvivuka vikwazo vyote vilivyokuwa vikikwamisha usajili wake,” chanzo cha habari kiliwaambia waandishi wetu.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic