August 1, 2015


Mshambuliaji aliyeonekana hafai Yanga, Said Bahanuzi, amesema amezaliwa upya na anayebisha akamtazame akichezea kikosi hicho.


Bahanuzi alitolewa kwa mkopo na Yanga kwenda Polisi Moro ambayo imeshuka daraja msimu uliopita, hivyo kuamua kuachana naye baada ya kubakiza mkataba wa mwaka mmoja.

Bahanuzi amesema amejipanga kuitumikia timu yake mpya kwa nguvu zote kuhakikisha inafanya vizuri katika msimu ujao wa Ligi Kuu Bara.

“Naomba uzima niweze kuisaidia timu yangu kwani ninachotakiwa kukifanya kwa upande wangu ni kuhakikisha najituma kwa nguvu zote ili kufanya vyema.

“Sasa nimezaliwa upya na nafanya vizuri mazoezini, hata katika mechi nitakuwa vizuri, watu wataona yale makali yangu yaliyopotea,” alisema Bahanuzi.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic