August 5, 2015

Kocha wa Bayern Munich Pep Guardiola amecharuka na kama si watu kuwahi, angeweza kuzichapa na kiungo wa AC Milan, mkongwe Nigel De Jong.


Pep alikuwa akimlalamikia kiungo huyo kumchezea rafu kiungo wake kinda Joshua Kimmich wakati timu hizo zilipokutana katika mechi ya michuano ya Audi Cup mjini Munich.
 
Kocha huyo alianza kumpa De Jong maneno makali, alimsisitiza si mtu makini aliyeshindwa hata kumuona kiungo huyo ni kinda ambaye anatakiwa kupewa moyo badala kuonyeshwa soka ni mchezo wa kikatili.
 
De Jong alicharuka baada ya Pep kukumbushia ile faulo yake ya fainali ya Kombe la Dunia mwaka 2010 alipomrukia tumboni Xabi Alonso ambaye sasa anakipiga Bayern Munich.

Hali hiyo ilimuudhi sana De Jong ambaye alitaka kumvaa Pep lakini wakaamuliwa wakati wakiingia vyumbani. Bayern ilishinda mechi hiyo kwa mabao 3-0.

KIMMICH (KULIA) KABLA YA KUUMIA SIKU HIYO.

FAINALI KOMBE LA DUNIA 2010







0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic