August 3, 2015

MAJIMAJI
Siku chache baada ya kocha wa Majimaji ya Songea iliyopanda Ligi Kuu Bara msimu huu, Raia wa Finland, Mike Lonnstrom, kuwasili nchini, ameweka wazi baadhi ya mikakati yake ndani ya timu hiyo ikiwemo kufanya usajili wa nguvu ili kujenga timu iwapo ataona kuna upungufu.


Kocha huyo raia wa Finland, alisema ana mikakati mizito ya kuifanya timu hiyo kuwa na uwezo wa kupambana na timu kubwa za hapa nchini, zikiwemo Azam, Simba na Yanga, hivyo atakaa na wachezaji wake na kuwaangalia, hasa safu ya ushambuliaji na kama hataridhika nao, basi atamtafuta mshambuliaji ambaye hana mbwembwe nyingi uwanjani, bali kazi yake ni kufunga tu.

Kocha huyo mwenye leseni A ya ukocha ya Shirikisho la Soka Ulaya (Uefa), alisema kuwa licha ya wengi kuamini kuwa mshambuliaji mzuri ni lazima awe mrefu, yeye hataangalia suala la urefu, bali atakachokiangalia ni uwezo wa kufunga tu.


“Kama nitakuta kuna tatizo la ushambuliaji, basi sitaenda mbali, nataangalia wa kumsajili kutoka hapahapa nchini, ila kawaida yangu siangalii umbo wala mbwembwe za mchezaji, bali kigezo kikubwa ninachokiangalia sana ni uwezo wake wa kufunga mabao, huyo ndiye nitapigania kumchukua,”  alisema Lonnstrom.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic