August 3, 2015


Na Said Mohammed, Zanzibar
Simba imeitwanga Jang’ombe Boys ya Zanzibar kwa mabao 3-0 katika mechi ya kirafiki iliyochezwa leo kwenye Uwanja wa Amaan mjini hapa.


Mabao ya Simba yamefungwa na Elius Maguri, dakika ya 14, Michael Mgimwa dakika ya 17 na Samir Omar katika dakika ya 81 na Kocha Dylan Kerr amesema angalau.

“Mechi ilikuwa nzuri, lakini kuna mambo kadhaa tunapaswa kubadilisha kama utumiaji wa nafasi tulizozipata.

“Tumetengeneza nyingi zaidi lakini tumefunga chache, ni vizuri kutumia nafasi kwa zaidi ya asilimia 70, sisi hatukufanya hivyo,” alisema Kerr raia wa Uingereza.


Hii ni mechi ya nne Simba inashinda mfululizo ikiwa visiwani hapa. Ilianza na kombaini ya Zanzibar 2-1, ikaituliza Black Sailors 4-0 na Polisi 2-0. Leo imemtungua mtu 3-0.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic