Vijana wa Simba wanaonekana wako siriaz na wamepania
kufanya vizuri ikiwezekana kupata namba katika kikosi cha kwanza.
Vijana hao wameonyesha makali yao wakati walipocheza mechi ya kirafiki dhidi ya Simba kubwa ambayo iliwafunga kwa mabao 2-0 katika mechi ya kirafiki kwenye Uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.
Lakini mmoja wa makinda hao aliokuwa akicheza nafasi
ya beki wa kati, alionekana hakuwa akitaka mchezo.
Mara kadhaa, alikuwa akiwagonga au kuwakwatua
washambuliaji wa Simba kubwa akiwemo nahodha Mussa Hassan Mgosi ambaye wakati
fulani alipitiwa na dogo huyo akalazimika kulala kwenye nyasi bandia za Uwanja
wa karume licha ya jua kuwa kali.
Wako wap sasa hawa vijana na faida ya kuwalea iko wap
ReplyDelete