November 25, 2015


Kipa wa Yanga, Deo Munish maarufu kama Dida amekuwa akijifua vilivyo akionyesha amepania hasa kurejea katika kikosi cha kwana.


Dida anajua kama atarejea katika kikosi cha kwanza, basi ana nafasi ya kucheza pia katika timu ya Tanzania Bara, Kili Stars au ile ya taifa, Taifa Stars.
 
Dida hana nafasi katika kikosi cha Yanga, Kili Stars au Taifa Stars ambazo aliwahi kuzichezea. Kwa sasa nafasi katika viko vyote viwili vya taifa ziko chini ya Aishi Manula na Ally Mustapha ambaye ndiye kipa namba moja wa Yanga.

Katika mazoezi ya Yanga, kipa huyo alikuwa akijifua kwa juhudi kubwa.
 

Pamoja na mazoezi mengine, alikuwa akiitumia nguzo ya goli kama sehemu ya mazoezi ili kuongeza wepesi wa mwili na kuufanya kuwa unaonyumbulika ambalo ni jambo jema kwa kipa.






0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic