November 25, 2015


Utaona katika kikosi cha Barcelona kuna kitu kimeongezeka tokea Luis Enrique aanze kazi.


Sasa inaonekana ni timu isiyoshikika, ngumu kuzuilika na haonekani wa kuizuia.

Lakini kama utapiga hesabu nzuri, unaona Bayern Munich chini ya Pep Guardiola inaweza kufanya hivyo, maana nayo ni kiwembe.

Zikiingia fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, basi huenda ikawa fainali tamu kuliko zikikutana timu nyingine au moja kati ya hizo na timu nyingine.

Barcelona imeitandika AS Roma kwa mabao 6-1 nyumbani kwao, lakini unajua namba mziki wa wakali kama Arjen Robben, Tomas Muller, Robert Lewandowski, Douglas Costa na Kingsley Coman ulivyo mgumu kuzuilika.

Kama timu hizo zitakutana fainali, kila mmoja atafurahia kuitazama fainali hiyo, maana itakuwa burudani ya aina yake.


Kwa mwenendo wa timu hizo kwa sasa, kila moja inaweza kufika fainali. Je, hazitakutana katikati? Ikiwa hivyo, itakuwa burudani bomba ya mwisho.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic