Kipa mkongwe nchini, Ivo Mapunda amejiunga na Azam FC.
Ivo atapewa mkataba wa mwaka mmoja na Mtedaji Mkuu wa Azam
FC, Saad Kawemba amesema kipa huyo amesajiliwa baada ya pendekezo la Kocha
Stewart Hall.
“Kocha alisema anataka kipa mzoefu nasi tukampa nafasi hiyo,”
alisema.
“Lakini mkataba hauwezi kuzidi mwaka mmoja kwa kuwa huenda
Ivo atakuwa na mipango yake mingine,” alisema.
Ivo aliomba kufanya mazoezi na kikosi cha Azam FC baada ya
kuachwa na Simba katika hatua za mwisho kabisa za usajili baada ya uongozi wa
Msimbazi, kusema alikuwa akiwasumbua licha ya kuwa wameishampa fedha za
usajili.
0 COMMENTS:
Post a Comment