Mshambuliaji wa zamani
wa Simba na Taifa Stars, Athumani Iddi Machuppa ameunga mkono kasi ya Rais John Magufuli
ambaye ameonyesha hataki mchezo.
Machuppa ameunga mkono
Serikali ya Magufuli kuvamia bandarini na kufanya ‘amshaamsha ya maana huku
abadhi ya viongozi wakiwemo wa TRA wakitimuliwa kazi.
Machuppa ambaye sasa
yuko nchini Sweden anakoendesha maisha yake ameeleza kusikitishwa na dhuruma
aliyowahi kufanyiwa bandarini huku akisisitiza lazima mali ya umma iogopwe.
Kupitia ukurasa wake wa
mtandao wa kijamii wa Facebook, Machuppa ameandika:
“Inabidi ifike mahala
mali ya umma iogopwe. Hao watu Bandarini washakula gari yangu mpya bila maelezo
wallah, malipo hapahapa duniani. Asante Kwa kusafisha Bandari.”
This comment has been removed by the author.
ReplyDelete:-d sasa hiyo gari alidhulumiwa vipi nae... ache uongo na wakina nani walumdhulumu
ReplyDeleteaeleze tu hiyo gari ili poteaje, labda ushuru ulimshinda ikapigwa mnada!