Straika
nyota wa Yanga, Mzimbabwe, Donald Ngoma, imeng’aa nchini Afrika Kusini na
tayari vigogo wa ligi kuu ya nchini humo, Mamelodi Sundowns FC wameonyesha nia
ya kumuwania.
Taarifa
hizo hazijamfurahisha hata kidogo Kocha Mkuu wa Yanga, Mholanzi, Hans van Der
Pluijm na tayari ameweka wazi msimamo na mikakati yake ya kuendelea kumbakiza
kundini mshambuliaji huyo mpaka mwisho wa msimu.
Taarifa
kutoka ndani ya Yanga zimeeleza kuwa, Mamelodi wamekuwa wakifurahishwa na
kiwango cha Ngoma na tayari kuna mazungumzo ya siri na uongozi wa Yanga
yanaendelea kwa ajili ya kumuachia nyota wao huyo aliyefunga mabao nane ndani
ya mechi tisa katika Ligi Kuu Bara, lakini suala la maelewano ya bei bado
halijawekwa mezani rasmi.
“Bado
mambo hayajaiva sawasawa lakini muelekeo ndiyo kama huo, Mamelodi wameonyesha
nia na kama kutakuwa na nguvu kubwa basi lolote linaweza kutokea ingawa mauzo
yake yatahusisha pande mbili, za uongozi na benchi la ufundi, wakiafikiana
kunaweza kuwa na biashara,” kilisema chanzo kwa sharti la kutotajwa jina.
Upande wa
Pluijm alipoulizwa na gazeti hili alisema: “Ni jambo zuri kwa mchezaji
kuhitajika kwingine lakini kwa kipindi hiki, siwezi kumuachia, siwezi kusema
kwamba naweza kumzuia moja kwa moja kwa sababu kila mtu ana akili yake lakini
bado namhitaji mpaka mwisho wa msimu.”
Taarifa za
wachezaji wa Yanga kuhitajika zaidi Sauz si mpya tena, kwa kuwa hivi karibuni
Mrisho Ngassa alisajiliwa Free State Stars na Mliberia, Kpah Sherman akatua
Mpumalanga Blac Aces na ikumbukwe kuwa kabla ya hapo Simon Msuva alifanya
majaribio kwa vinara wa ligi ya Sauz, Bidvest Wits.
0 COMMENTS:
Post a Comment