Katibu Mkuu wa Wizara ya Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo,
Profesa Elisante Ole Gabriel leo amefunga program ya Live Your Goal
iliyoandaliwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu nchini (TFF) katika uwanja wa
Karume jijini Dar es salaam.
Ole Gabriel amewashukuru vijana waliojitokeza kushiriki katika
program hiyo na kuwaomba wazazi kuwarushu watoto wa kike kujtokeza na kushiriki
katika program hiyo ya kuhamasisha wanawake kucheza mpira wa miguu.
Live
Your Goal ni program inayoendeshwa na TFF kwa msaada kutoka FIFA yenye lengo la
kuwahamasisha watoto wa kike, na wasichana kujitokeza kuucheza na kuupenda
mpira wa miguu.
Programu
hii iliyomalizika leo imejumuisha vilabu sita vya wanawake, kutoka wilaya za
Ilala, Kinodoni na Temeke, shule za msingi sita kutoka jijini Dar es salaam
ambapo washiriki walikua wanafunzi wenye umri kaunzia miaka 8 na kuendelea, na
ikifanyika kwa mara ya pili baada ya awalia mwezi Juni mwaka huu mkoani Geita.
0 COMMENTS:
Post a Comment