November 28, 2015


Kili Stars itashuka dimbani Jumatatu kupambana na wenyeji Ethiopia katika mechi ya robo fainali.

Wakati Stars imeingia robo fainali kama kinara wa Kundi A, Ethiopia imetumia ‘mlango wa uani’ maarufu kama best looser baada ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Stars, leo.

Stars ilishinda mechi zake mbili za hatua ya makundi na kutoka sare dhidi ya Ethiopia.

Mechi hiyo ya Jumatatu inatarajiwa kuwa ngumu kwa kuwa Ethiopia ambao wameonyesha wazi hawana kikosi imara, watakuwa wameongeza hali ya kujiamini baada ya sare hiyo iliyowavuja hadi robo fainali.

Hata hivyo, Kocha Mkuu wa Kili Stars, Abdallah Kibadeni amesema ana imani na kikosi chake.

“Tulicheza vizuri, sema limetokea kosa na wao wamelitumia kupata bao. Lakini tunakutana nao tena hatua ya robo fainali.
“Mechi itakuwa ngumu kwa kuwa wako nyumbani kama wenyeji, lakini tutapambana kwa kuwa tumetumwa na Watanzania,” alisema.

.

0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic