Katika harakati ya kujiweka sawa, Simba kesho Jumapili inakwenda visiwani
Zanzibar kuweka kambi huku Kocha Dylan Kerr, akifurahia ushambuliaji pacha wa
Danny Lyanga na Hija Ugando.
Mabosi wa Simba wamepiga hesabu na kuona
Zanzibar ni mahali pazuri panapofaa kwa kambi yao ya muda kuelekea mechi na
Azam ambayo inatajwa kuamua hatma ya Kerr kama atabaki au vinginevyo.
Kerr amesema kuwa:
“Tunaenda Zanzibar Jumapili (kesho) kuweka kambi ya siku 10 kabla ya mchezo
wetu na Azam, naamini kambi hii itatusaidia kupata kitu tofauti kwani tunacheza
na timu nzuri.”
Wakati huohuo, Kerr ameonyesha wazi furaha yake
kutokana na uwezo mkubwa ulionyeshwa na mastraika wake Hija Ugando na Danny
Lyanga.
Katika mazoezi hayo yaliyofanyika jana Ijumaa
kwenye Uwanja wa Karume, Dar, Kerr
aliwachezesha pamoja washambuliaji hao ambao walionyesha uwelewano mkubwa.
Ugando ambaye yupo majaribio katika kipindi
hiki akisubiri majibu ya majaribio kwenye kikosi cha Atalanta ya Ligi Kuu
Italia, alionekana kuwa bora zaidi kwa kufunga mabao matatu katika mazoezi hayo
huku yote akitengenezewa na Lyanga.
“Nimefurahishwa nao kwa sababu walikuwa
wakicheza kwa kuelewana na wametengeneza nafasi nyingi licha ya kufanikiwa
kufunga mabao matatu.
“Nadhani watanisaidia ingawa bado ni mapema
kutolea uamuzi kwa sababu yule Ugando bado yupo katika majaribio ila
nimefurahishwa na walichokifanya leo,” alisema Kerr.
0 COMMENTS:
Post a Comment