Simba imeendelea na mazoezi chini ya Kocha Dylan Kerr na
msaidizi wake, Iddi Salim. Mazoezi hayo yamefanyika kwenye Uwanja wa Karume Ilala jijini Dar es Salaam, leo.
Mazoezi ya Simba yamekuwa makali sana na ilikuwa mazoezi
mechi kati ya timu kubwa dhidi ya vijana ya Simba, mechi ambayo iliishia kwa wakubwa kushinda kwa mabao 2-0.
Kati ya waliokuwa wakijifua, mmoja wapo alikuwa
ni Mganda Brian Majegwa ambaye tayari ameonyesha nia ya kuichezea Simba na
kuachana na Azam FC.
Mazoezi hayo yalikuwa na ushindani mkubwa huku kila upande
ukionekana umepania kushinda hasa.
Simba iko katika maandalizi kujiweka sawa kwa ajili ya Ligi
Kuu Bara iliyokuwa imesimama kwa muda.
ANGALIA PICHAZEEEE.
0 COMMENTS:
Post a Comment