December 1, 2015


Klabu ya Ligi Kuu ya Denmark inayomtaka kiungo nyota wa Azam FC, Farid Musa ni katika klabu zinazosajili Waafrika wachache lakini wamekuwa na mafanikio.


Brondy IF iliyoanzishwa mwaka 1964 ni moja ya timu bora nchini Denmark na kwa kipindi cha miaka 10 sasa imekuwa na mafanikio kwa asilimia kubwa ingawa si asilimia ya juu sana.

MASHABIKI WA BRONDY WAKIIUNGA MKONO TIMU YAO.

Wachezaji ambao walitokea Afrika na kufanya vizuri sana katika kikosi hicho ni pamoja na Uche Okwuchukwu aliyetokea Nigeria, Ousman Jallow (Gambia) na nahidha wa muda mrefu wa Zambia, Chris Katongo.

Wachezaji wengi wa kikosi hicho wamekuwa wakisajiliwa kutoka nchini Denmark.

Angalau nchi za jirani za Norway, Sweden na Finland nazo zimekuwa na wachezaji wengi katika kikosi hicho cha Brondy IF.


0 COMMENTS:

Post a Comment

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic