Kiungo nyota wa Barcelona,
Neymar Jr, ameonyesha wazi kutofurahishwa na kuwepo kwa Cristiano Ronaldo
katika wachezaji watatu walioingia fainali ya kuwania mchezaji bora wa dunia
maarufu kama Ballon d’Or.
Watatu walioingia
fainali ni yeye Neymar, Lionel Messi na Ronaldo wenye ushindani
mkubwa.
Ingawa Neymar hajaenda moja kwa moja kusema Ronaldo
asingeingia, lakini kauli yake kwamba Luis Suarez alistahili kuingia fainali,
maana yake Ronaldo hakupaswa kuingia.
Pamoja na Neymar kuingia, Messi na Ronaldo bado wanaonekana
kuendelea kuwa gumzo.
Lakini pia kufanya vizuri kwa Neymar mwishoni kunaonekana
kuwa changamoto kwa wote hao wawili.
0 COMMENTS:
Post a Comment