Kocha Mkuu wa Yanga,
Hans van der Pluijm ameendelea kukifua kikosi chake katika Uwanja wa Boko
Veterani.
Pluijm zaidi alionekana
kuwafundisha wachezaji wake kucheza kwa kasi huku akisisitiza suala la umakini.
Mara nyingi, Pluijm
raia wa Uholanzi alikuwa akisisitiza suala la kuhakikisha hawapotezi pasi.
“Lazima uwe makini,
piga pasi za uhakika na hakikisha unalinda mpira,” alisema akisisitiza.
Mara kadhaa,
aliwaonyesha namna ya kukimbia na nini cha kufanya ili kuhakikisha wanatimiza
malengo.
0 COMMENTS:
Post a Comment