Sergio Ramos ametangwa
kuwa beki bora wa La Liga kwa msimu wa 2014-2015 katika sherehe za utoaji tuzo
zilizofanyika jijini Barcelona usiku wa kuamkia leo.
Ramos amewapiga
kumbo mabeki wawili nyota Piqué wa Barcelona na Otamendi aliyekuwa akikipiga
Valencia lakini sasa yuko Man City ya England.
Baada ya
kuchukua tuzo, Ramos aliwashukuru wachezaji wenzake na benchi la ufundi la
Madrid kumuwezesha kubeba tuzo hiyo.
Naye kiungo
kinda, James Rodrigues ambaye ndiyo msimu wake wa kwanza Madrid ameshinda tuzo
ya kiungo bora wa La Liga kwa msimu wa 2014-2015.
James amewapiga
kumbo wakongwe wa La Liga kama Antoine Griezmann wa Atletico Madrid na Andres Iniesta
wa Barcelona.
0 COMMENTS:
Post a Comment