February 14, 2016

Kocha aliyetupiwa virago Simba, Dylan Kerr ameibukia katika klabu ya Manchester City.

Kerr ametupia picha mtandaoni akiwa katika ofisi za klabu ya Manchester City pamoja na uwanja wa klabu hiyo wa Etihad.

Hata hivyo haikujulikana mara moja, alikuwa amefika kwenye ofisi za klabu hiyo huku akionekana na baadhi ya maofisa wa Man City kwa sababu zipi.

Juhudi za kumsaka Kerr hazijafanikiwa, lakini tunaendelea kumsaka ili kujua alikuwa katika matembezi ya kawaida tu au kuna jambo.

Kerr aliondolewa na nafasi yake kuchukuliwa na Jackson Mayanja raia wa Uganda ambaye ameshinda mechi saba mfululizo tokea hapo. Sita za Ligi Kuu Bara na moja ya Kombe la Shiriksho. 



1 COMMENTS:

  1. Huko ni nyumbani kwao na hao maofisa wa etihad ni wenzake,kwani wewe huwezi kwenda jangwani au Msimbazina kuzungumza na maafisa wa Yanga au Simba?Sidhani kama kuonekana kwake hapo Etihad ni habari.Labda Ungemuona Guadiola etihad hiyo ingeweza kuwa habari kwa sababu ndiye kocha anayesubiriwa kuanza Kazi hapo Etihad

    ReplyDelete

TwitterFacebookGoogle PlusLinkedInRSS FeedEmail

GONGA HAPA KWENDA AZAM TV

B2.jpg
Image and video hosting by TinyPic